Katika mafunzo yetu ya leo tutazungumzia Mambo matatu ya msingi na ya muhimu unayotakiwa kuyafanya

katika mtandao ili uweze kupata wateja kwa wingi na kwa kiingereza tunaita mambo haya matatu “The three C’s of Marketing”.

C ya kwanza ni Create traffic: Unatakiwa kuonekana mbele ya macho ya watu wengi. Kuna tofauti kubwa

kama watakuona watu 10 kwa siku na watu 1000 kwa siku, Ni wazi kabisa kwamba wakikuona watu wengi

mauzo nayo yatakuwa mengi zaidi. Ukishatengeneza traffic hautangazi bidhaa unazouza au huduma

unazotoa bali unatangaza SUMAKU. Sumaku ni zawadi ambayo unaitangaza kwa wateja wako watarajiwa.

Kwa mfano kama unataka kuuza cream za kuondoa chunusi usoni badala ya kutangaza cream yako,

unawaambia Kama una tatizo la chunusi la muda mrefu basi nimeandaa Group ya WhatsApp ambayo

inafundisha namna ya kuondoa chunusi sugu ndani ya siku tatu kama unataka kujifunza karibu katika group

yetu na andika namba yako chini. Hiyo ndiyo Sumaku na ndio maana unawanasa watu.

C ya pili ni Capture Leads: Katika hatua hii tunakusanya taarifa zao Jina, namba ya simu na email. Na

ukishapata taarifa zao unaanza kuwasiliana nao kupitia jukwaa lako. Katika kuwasiliana nao unatakiwa

kujenga uaminifu, unajenga ukaribu kwao na unawafundisha ili kujenga trust. Na ukishafanya hivyo ndio

tunakuja kwenye C ya mwisho.

C ya tatu ni Convert sales: Hatua hii ndio unatangaza bidhaa au huduma unazotoa. Mwisho unaweza

kuwaambia kama nilivyosema katika mafunzo ya leo tumeona kuwa zipo cream maalumu ambazo zinaweza

kuondoa chunusi ndani ya muda mfupi. Na cream ambazo na nakushauri utumie ni cream za aina fulani.

Kama ungependa kupata hii cream unaweza kunijulisha na pia utambue kuwa cream zilizobaki ni chache na

ukichukua cream sasa hivi nitakupa na bonus ya kitu .  Hapa unaonyesha kuwa una nia safi ya kumsaidia. Na

kama unayo ofa mpe ofa kwa sababu huyo mteja hajawahi kununua kabla kutoka kwako. Kwa hiyo ni vizuri

mauzo ya kwanza ukatoa na ofa au Discount (punguzo la bei), kufanya hivyo itakusaidia sana kuuza.

Kwa hiyo mambo matatu ya kufanya katika mtandao ili kupata wateja kwa wingi ni Create traffic- hapa

unaweza kutumia facebook au instagram kwa kulipia matangazo kwa kuwalenga watu husika unaowahitaji

kama vijana, wanawake au wakurugenzi wa kampuni. Pili unakusanya taarifa zao na mwisho unafanya

mauzo.

Kama una swali au maoni juu ya makala hii basi acha comment yako na usisahau kuwashirikisha wengine ili nao wanufaike na mafunzo haya mazuri na muhimu sana kwao kwa kubonyeza vitufe vya mitandao ya kijamii hapo chini.


Abdallah Hemedi
Abdallah Hemedi

Content Manager

Ujumbe Wa Facebook

Leave a Reply

Your email address will not be published.